Swahili
Surah Al-Qamar ( The Moon ) - Aya count 55
اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ 
( 1 ) 
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ 
( 2 ) 
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
وَكَذَّبُوا وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ 
( 3 ) 
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّنَ الْأَنبَاءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ 
( 4 ) 
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
حِكْمَةٌ بَالِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ النُّذُرُ 
( 5 ) 
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ الدَّاعِ إِلَىٰ شَيْءٍ نُّكُرٍ 
( 6 ) 
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
خُشَّعًا أَبْصَارُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ مُّنتَشِرٌ 
( 7 ) 
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
مُّهْطِعِينَ إِلَى الدَّاعِ ۖ يَقُولُ الْكَافِرُونَ هَٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ 
( 8 ) 
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا عَبْدَنَا وَقَالُوا مَجْنُونٌ وَازْدُجِرَ 
( 9 ) 
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
فَدَعَا رَبَّهُ أَنِّي مَغْلُوبٌ فَانتَصِرْ 
( 10 ) 
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
فَفَتَحْنَا أَبْوَابَ السَّمَاءِ بِمَاءٍ مُّنْهَمِرٍ 
( 11 ) 
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
وَفَجَّرْنَا الْأَرْضَ عُيُونًا فَالْتَقَى الْمَاءُ عَلَىٰ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ 
( 12 ) 
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
وَحَمَلْنَاهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَاحٍ وَدُسُرٍ 
( 13 ) 
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
تَجْرِي بِأَعْيُنِنَا جَزَاءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ 
( 14 ) 
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
وَلَقَد تَّرَكْنَاهَا آيَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ 
( 15 ) 
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ 
( 16 ) 
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ 
( 17 ) 
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ 
( 18 ) 
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِي يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ 
( 19 ) 
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
تَنزِعُ النَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ 
( 20 ) 
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ 
( 21 ) 
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ 
( 22 ) 
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِالنُّذُرِ 
( 23 ) 
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
فَقَالُوا أَبَشَرًا مِّنَّا وَاحِدًا نَّتَّبِعُهُ إِنَّا إِذًا لَّفِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ 
( 24 ) 
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
أَأُلْقِيَ الذِّكْرُ عَلَيْهِ مِن بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ 
( 25 ) 
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ الْكَذَّابُ الْأَشِرُ 
( 26 ) 
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
إِنَّا مُرْسِلُو النَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَارْتَقِبْهُمْ وَاصْطَبِرْ 
( 27 ) 
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ الْمَاءَ قِسْمَةٌ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ 
( 28 ) 
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
فَنَادَوْا صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ 
( 29 ) 
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ 
( 30 ) 
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَاحِدَةً فَكَانُوا كَهَشِيمِ الْمُحْتَظِرِ 
( 31 ) 
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ 
( 32 ) 
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ بِالنُّذُرِ 
( 33 ) 
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّا آلَ لُوطٍ ۖ نَّجَّيْنَاهُم بِسَحَرٍ 
( 34 ) 
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي مَن شَكَرَ 
( 35 ) 
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا بِالنُّذُرِ 
( 36 ) 
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
وَلَقَدْ رَاوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِ فَطَمَسْنَا أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ 
( 37 ) 
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ 
( 38 ) 
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ 
( 39 ) 
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ 
( 40 ) 
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
وَلَقَدْ جَاءَ آلَ فِرْعَوْنَ النُّذُرُ 
( 41 ) 
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَاهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ 
( 42 ) 
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُولَٰئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَاءَةٌ فِي الزُّبُرِ 
( 43 ) 
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ 
( 44 ) 
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
سَيُهْزَمُ الْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ الدُّبُرَ 
( 45 ) 
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
بَلِ السَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَالسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ 
( 46 ) 
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ 
( 47 ) 
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ 
( 48 ) 
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ 
( 49 ) 
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
وَمَا أَمْرُنَا إِلَّا وَاحِدَةٌ كَلَمْحٍ بِالْبَصَرِ 
( 50 ) 
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ 
( 51 ) 
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
وَكُلُّ شَيْءٍ فَعَلُوهُ فِي الزُّبُرِ 
( 52 ) 
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
وَكُلُّ صَغِيرٍ وَكَبِيرٍ مُّسْتَطَرٌ 
( 53 ) 
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَهَرٍ 
( 54 ) 
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍ 
( 55 ) 
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.