Swahili
Surah Al-Haaqqah ( The Inevitable ) - Aya count 52
الْحَاقَّةُ 
( 1 ) 
Tukio la haki.
مَا الْحَاقَّةُ 
( 2 ) 
Nini hilo Tukio la haki?
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْحَاقَّةُ 
( 3 ) 
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
كَذَّبَتْ ثَمُودُ وَعَادٌ بِالْقَارِعَةِ 
( 4 ) 
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهْلِكُوا بِالطَّاغِيَةِ 
( 5 ) 
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
وَأَمَّا عَادٌ فَأُهْلِكُوا بِرِيحٍ صَرْصَرٍ عَاتِيَةٍ 
( 6 ) 
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
سَخَّرَهَا عَلَيْهِمْ سَبْعَ لَيَالٍ وَثَمَانِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومًا فَتَرَى الْقَوْمَ فِيهَا صَرْعَىٰ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ خَاوِيَةٍ 
( 7 ) 
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
فَهَلْ تَرَىٰ لَهُم مِّن بَاقِيَةٍ 
( 8 ) 
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
وَجَاءَ فِرْعَوْنُ وَمَن قَبْلَهُ وَالْمُؤْتَفِكَاتُ بِالْخَاطِئَةِ 
( 9 ) 
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
فَعَصَوْا رَسُولَ رَبِّهِمْ فَأَخَذَهُمْ أَخْذَةً رَّابِيَةً 
( 10 ) 
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
إِنَّا لَمَّا طَغَى الْمَاءُ حَمَلْنَاكُمْ فِي الْجَارِيَةِ 
( 11 ) 
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
لِنَجْعَلَهَا لَكُمْ تَذْكِرَةً وَتَعِيَهَا أُذُنٌ وَاعِيَةٌ 
( 12 ) 
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
فَإِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ نَفْخَةٌ وَاحِدَةٌ 
( 13 ) 
Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
وَحُمِلَتِ الْأَرْضُ وَالْجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةً وَاحِدَةً 
( 14 ) 
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
فَيَوْمَئِذٍ وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ 
( 15 ) 
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
وَانشَقَّتِ السَّمَاءُ فَهِيَ يَوْمَئِذٍ وَاهِيَةٌ 
( 16 ) 
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
وَالْمَلَكُ عَلَىٰ أَرْجَائِهَا ۚ وَيَحْمِلُ عَرْشَ رَبِّكَ فَوْقَهُمْ يَوْمَئِذٍ ثَمَانِيَةٌ 
( 17 ) 
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
يَوْمَئِذٍ تُعْرَضُونَ لَا تَخْفَىٰ مِنكُمْ خَافِيَةٌ 
( 18 ) 
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ فَيَقُولُ هَاؤُمُ اقْرَءُوا كِتَابِيَهْ 
( 19 ) 
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَاقٍ حِسَابِيَهْ 
( 20 ) 
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ 
( 21 ) 
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ 
( 22 ) 
Katika Bustani ya juu,
قُطُوفُهَا دَانِيَةٌ 
( 23 ) 
Matunda yake yakaribu.
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا أَسْلَفْتُمْ فِي الْأَيَّامِ الْخَالِيَةِ 
( 24 ) 
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِشِمَالِهِ فَيَقُولُ يَا لَيْتَنِي لَمْ أُوتَ كِتَابِيَهْ 
( 25 ) 
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيَهْ 
( 26 ) 
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
يَا لَيْتَهَا كَانَتِ الْقَاضِيَةَ 
( 27 ) 
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
مَا أَغْنَىٰ عَنِّي مَالِيَهْ ۜ 
( 28 ) 
Mali yangu hayakunifaa kitu.
هَلَكَ عَنِّي سُلْطَانِيَهْ 
( 29 ) 
Madaraka yangu yamenipotea.
خُذُوهُ فَغُلُّوهُ 
( 30 ) 
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
ثُمَّ الْجَحِيمَ صَلُّوهُ 
( 31 ) 
Kisha mtupeni Motoni!
ثُمَّ فِي سِلْسِلَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعًا فَاسْلُكُوهُ 
( 32 ) 
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
إِنَّهُ كَانَ لَا يُؤْمِنُ بِاللَّهِ الْعَظِيمِ 
( 33 ) 
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ 
( 34 ) 
Wala hahimizi kulisha masikini.
فَلَيْسَ لَهُ الْيَوْمَ هَاهُنَا حَمِيمٌ 
( 35 ) 
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنْ غِسْلِينٍ 
( 36 ) 
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
لَّا يَأْكُلُهُ إِلَّا الْخَاطِئُونَ 
( 37 ) 
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
فَلَا أُقْسِمُ بِمَا تُبْصِرُونَ 
( 38 ) 
Basi naapa kwa mnavyo viona,
وَمَا لَا تُبْصِرُونَ 
( 39 ) 
Na msivyo viona,
إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ 
( 40 ) 
Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَاعِرٍ ۚ قَلِيلًا مَّا تُؤْمِنُونَ 
( 41 ) 
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
وَلَا بِقَوْلِ كَاهِنٍ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ 
( 42 ) 
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ 
( 43 ) 
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
وَلَوْ تَقَوَّلَ عَلَيْنَا بَعْضَ الْأَقَاوِيلِ 
( 44 ) 
Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
لَأَخَذْنَا مِنْهُ بِالْيَمِينِ 
( 45 ) 
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
ثُمَّ لَقَطَعْنَا مِنْهُ الْوَتِينَ 
( 46 ) 
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
فَمَا مِنكُم مِّنْ أَحَدٍ عَنْهُ حَاجِزِينَ 
( 47 ) 
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
وَإِنَّهُ لَتَذْكِرَةٌ لِّلْمُتَّقِينَ 
( 48 ) 
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
وَإِنَّا لَنَعْلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ 
( 49 ) 
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
وَإِنَّهُ لَحَسْرَةٌ عَلَى الْكَافِرِينَ 
( 50 ) 
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
وَإِنَّهُ لَحَقُّ الْيَقِينِ 
( 51 ) 
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ 
( 52 ) 
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.