Swahili
Surah Al-Waqi'ah ( The Event ) - Aya count 96
إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ 
( 1 ) 
Litakapo tukia hilo Tukio
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ 
( 2 ) 
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ 
( 3 ) 
Literemshalo linyanyualo,
إِذَا رُجَّتِ الْأَرْضُ رَجًّا 
( 4 ) 
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا 
( 5 ) 
Na milima itapo sagwasagwa,
فَكَانَتْ هَبَاءً مُّنبَثًّا 
( 6 ) 
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
وَكُنتُمْ أَزْوَاجًا ثَلَاثَةً 
( 7 ) 
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ 
( 8 ) 
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ 
( 9 ) 
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ 
( 10 ) 
Na wa mbele watakuwa mbele.
أُولَٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ 
( 11 ) 
Hao ndio watakao karibishwa
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ 
( 12 ) 
Katika Bustani zenye neema.
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ 
( 13 ) 
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ 
( 14 ) 
Na wachache katika wa mwisho.
عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ 
( 15 ) 
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
مُّتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ 
( 16 ) 
Wakiviegemea wakielekeana.
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ 
( 17 ) 
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ 
( 18 ) 
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ 
( 19 ) 
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ 
( 20 ) 
Na matunda wayapendayo,
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ 
( 21 ) 
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
وَحُورٌ عِينٌ 
( 22 ) 
Na Mahurulaini,
كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ 
( 23 ) 
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ 
( 24 ) 
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا 
( 25 ) 
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا 
( 26 ) 
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ 
( 27 ) 
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ 
( 28 ) 
Katika mikunazi isiyo na miba,
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ 
( 29 ) 
Na migomba iliyo pangiliwa,
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ 
( 30 ) 
Na kivuli kilicho tanda,
وَمَاءٍ مَّسْكُوبٍ 
( 31 ) 
Na maji yanayo miminika,
وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ 
( 32 ) 
Na matunda mengi,
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ 
( 33 ) 
Hayatindikii wala hayakatazwi,
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ 
( 34 ) 
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاءً 
( 35 ) 
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا 
( 36 ) 
Na tutawafanya vijana,
عُرُبًا أَتْرَابًا 
( 37 ) 
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ 
( 38 ) 
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ 
( 39 ) 
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ 
( 40 ) 
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ 
( 41 ) 
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
فِي سَمُومٍ وَحَمِيمٍ 
( 42 ) 
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ 
( 43 ) 
Na kivuli cha moshi mweusi,
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ 
( 44 ) 
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ 
( 45 ) 
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ 
( 46 ) 
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ 
( 47 ) 
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ 
( 48 ) 
Au baba zetu wa zamani?
قُلْ إِنَّ الْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ 
( 49 ) 
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ 
( 50 ) 
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ 
( 51 ) 
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ 
( 52 ) 
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ 
( 53 ) 
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ 
( 54 ) 
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ 
( 55 ) 
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ 
( 56 ) 
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ 
( 57 ) 
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
أَفَرَأَيْتُم مَّا تُمْنُونَ 
( 58 ) 
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
أَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ 
( 59 ) 
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ 
( 60 ) 
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ 
( 61 ) 
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ 
( 62 ) 
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ 
( 63 ) 
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ 
( 64 ) 
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ 
( 65 ) 
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ 
( 66 ) 
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ 
( 67 ) 
Bali sisi tumenyimwa.
أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاءَ الَّذِي تَشْرَبُونَ 
( 68 ) 
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
أَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ 
( 69 ) 
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
لَوْ نَشَاءُ جَعَلْنَاهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ 
( 70 ) 
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ 
( 71 ) 
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
أَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِئُونَ 
( 72 ) 
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَةً وَمَتَاعًا لِّلْمُقْوِينَ 
( 73 ) 
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ 
( 74 ) 
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ 
( 75 ) 
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ 
( 76 ) 
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ 
( 77 ) 
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ 
( 78 ) 
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ 
( 79 ) 
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ 
( 80 ) 
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَفَبِهَٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ 
( 81 ) 
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ 
( 82 ) 
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ 
( 83 ) 
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ 
( 84 ) 
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ 
( 85 ) 
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ 
( 86 ) 
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ 
( 87 ) 
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ 
( 88 ) 
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ 
( 89 ) 
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ 
( 90 ) 
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ 
( 91 ) 
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ 
( 92 ) 
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ 
( 93 ) 
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ 
( 94 ) 
Na kutiwa Motoni.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ 
( 95 ) 
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ 
( 96 ) 
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.