Swahili
Surah Ash-Shams ( The Sun ) - Aya count 15
وَالشَّمْسِ وَضُحَاهَا 
( 1 ) 
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
وَالْقَمَرِ إِذَا تَلَاهَا 
( 2 ) 
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
وَالنَّهَارِ إِذَا جَلَّاهَا 
( 3 ) 
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَاهَا 
( 4 ) 
Na kwa usiku unapo lifunika!
وَالسَّمَاءِ وَمَا بَنَاهَا 
( 5 ) 
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
وَالْأَرْضِ وَمَا طَحَاهَا 
( 6 ) 
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّاهَا 
( 7 ) 
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا 
( 8 ) 
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا 
( 9 ) 
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّاهَا 
( 10 ) 
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَاهَا 
( 11 ) 
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
إِذِ انبَعَثَ أَشْقَاهَا 
( 12 ) 
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ اللَّهِ نَاقَةَ اللَّهِ وَسُقْيَاهَا 
( 13 ) 
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنبِهِمْ فَسَوَّاهَا 
( 14 ) 
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
وَلَا يَخَافُ عُقْبَاهَا 
( 15 ) 
Wala Yeye haogopi matokeo yake.