Swahili
Surah Ar-Rahman ( The Most Graciouse ) - Aya count 78
الرَّحْمَٰنُ 
( 1 ) 
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
عَلَّمَ الْقُرْآنَ 
( 2 ) 
Amefundisha Qur'ani.
خَلَقَ الْإِنسَانَ 
( 3 ) 
Amemuumba mwanaadamu,
عَلَّمَهُ الْبَيَانَ 
( 4 ) 
Akamfundisha kubaini.
الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ بِحُسْبَانٍ 
( 5 ) 
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
وَالنَّجْمُ وَالشَّجَرُ يَسْجُدَانِ 
( 6 ) 
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
وَالسَّمَاءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ الْمِيزَانَ 
( 7 ) 
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
أَلَّا تَطْغَوْا فِي الْمِيزَانِ 
( 8 ) 
Ili msidhulumu katika mizani.
وَأَقِيمُوا الْوَزْنَ بِالْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا الْمِيزَانَ 
( 9 ) 
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
وَالْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ 
( 10 ) 
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
فِيهَا فَاكِهَةٌ وَالنَّخْلُ ذَاتُ الْأَكْمَامِ 
( 11 ) 
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
وَالْحَبُّ ذُو الْعَصْفِ وَالرَّيْحَانُ 
( 12 ) 
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 13 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
خَلَقَ الْإِنسَانَ مِن صَلْصَالٍ كَالْفَخَّارِ 
( 14 ) 
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
وَخَلَقَ الْجَانَّ مِن مَّارِجٍ مِّن نَّارٍ 
( 15 ) 
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 16 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
رَبُّ الْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ الْمَغْرِبَيْنِ 
( 17 ) 
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 18 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مَرَجَ الْبَحْرَيْنِ يَلْتَقِيَانِ 
( 19 ) 
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
بَيْنَهُمَا بَرْزَخٌ لَّا يَبْغِيَانِ 
( 20 ) 
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 21 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَخْرُجُ مِنْهُمَا اللُّؤْلُؤُ وَالْمَرْجَانُ 
( 22 ) 
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 23 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَلَهُ الْجَوَارِ الْمُنشَآتُ فِي الْبَحْرِ كَالْأَعْلَامِ 
( 24 ) 
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 25 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ 
( 26 ) 
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ 
( 27 ) 
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 28 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَسْأَلُهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِي شَأْنٍ 
( 29 ) 
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 30 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
سَنَفْرُغُ لَكُمْ أَيُّهَ الثَّقَلَانِ 
( 31 ) 
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 32 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يَا مَعْشَرَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ إِنِ اسْتَطَعْتُمْ أَن تَنفُذُوا مِنْ أَقْطَارِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ فَانفُذُوا ۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلْطَانٍ 
( 33 ) 
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 34 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يُرْسَلُ عَلَيْكُمَا شُوَاظٌ مِّن نَّارٍ وَنُحَاسٌ فَلَا تَنتَصِرَانِ 
( 35 ) 
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 36 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فَإِذَا انشَقَّتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ وَرْدَةً كَالدِّهَانِ 
( 37 ) 
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 38 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُسْأَلُ عَن ذَنبِهِ إِنسٌ وَلَا جَانٌّ 
( 39 ) 
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 40 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
يُعْرَفُ الْمُجْرِمُونَ بِسِيمَاهُمْ فَيُؤْخَذُ بِالنَّوَاصِي وَالْأَقْدَامِ 
( 41 ) 
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 42 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
هَٰذِهِ جَهَنَّمُ الَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا الْمُجْرِمُونَ 
( 43 ) 
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
يَطُوفُونَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ حَمِيمٍ آنٍ 
( 44 ) 
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 45 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ جَنَّتَانِ 
( 46 ) 
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 47 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ذَوَاتَا أَفْنَانٍ 
( 48 ) 
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 49 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا عَيْنَانِ تَجْرِيَانِ 
( 50 ) 
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 51 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَاكِهَةٍ زَوْجَانِ 
( 52 ) 
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 53 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ فُرُشٍ بَطَائِنُهَا مِنْ إِسْتَبْرَقٍ ۚ وَجَنَى الْجَنَّتَيْنِ دَانٍ 
( 54 ) 
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 55 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِنَّ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ 
( 56 ) 
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 57 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
كَأَنَّهُنَّ الْيَاقُوتُ وَالْمَرْجَانُ 
( 58 ) 
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 59 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
هَلْ جَزَاءُ الْإِحْسَانِ إِلَّا الْإِحْسَانُ 
( 60 ) 
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 61 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ 
( 62 ) 
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 63 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُدْهَامَّتَانِ 
( 64 ) 
Za kijani kibivu.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 65 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا عَيْنَانِ نَضَّاخَتَانِ 
( 66 ) 
Na chemchem mbili zinazo furika.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 67 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِمَا فَاكِهَةٌ وَنَخْلٌ وَرُمَّانٌ 
( 68 ) 
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 69 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
فِيهِنَّ خَيْرَاتٌ حِسَانٌ 
( 70 ) 
Humo wamo wanawake wema wazuri.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 71 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
حُورٌ مَّقْصُورَاتٌ فِي الْخِيَامِ 
( 72 ) 
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 73 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ 
( 74 ) 
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 75 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ رَفْرَفٍ خُضْرٍ وَعَبْقَرِيٍّ حِسَانٍ 
( 76 ) 
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ 
( 77 ) 
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
تَبَارَكَ اسْمُ رَبِّكَ ذِي الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ 
( 78 ) 
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.