Swahili
Surah Al-A'la ( The Most High ) - Aya count 19
سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى 
( 1 ) 
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
الَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ 
( 2 ) 
Aliye umba, na akaweka sawa,
وَالَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ 
( 3 ) 
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
وَالَّذِي أَخْرَجَ الْمَرْعَىٰ 
( 4 ) 
Na aliye otesha malisho,
فَجَعَلَهُ غُثَاءً أَحْوَىٰ 
( 5 ) 
Kisha akayafanya makavu, meusi.
سَنُقْرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰ 
( 6 ) 
Tutakusomesha wala hutasahau,
إِلَّا مَا شَاءَ اللَّهُ ۚ إِنَّهُ يَعْلَمُ الْجَهْرَ وَمَا يَخْفَىٰ 
( 7 ) 
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
وَنُيَسِّرُكَ لِلْيُسْرَىٰ 
( 8 ) 
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
فَذَكِّرْ إِن نَّفَعَتِ الذِّكْرَىٰ 
( 9 ) 
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخْشَىٰ 
( 10 ) 
Atakumbuka mwenye kuogopa.
وَيَتَجَنَّبُهَا الْأَشْقَى 
( 11 ) 
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
الَّذِي يَصْلَى النَّارَ الْكُبْرَىٰ 
( 12 ) 
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ 
( 13 ) 
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
قَدْ أَفْلَحَ مَن تَزَكَّىٰ 
( 14 ) 
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
وَذَكَرَ اسْمَ رَبِّهِ فَصَلَّىٰ 
( 15 ) 
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
بَلْ تُؤْثِرُونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا 
( 16 ) 
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
وَالْآخِرَةُ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ 
( 17 ) 
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
إِنَّ هَٰذَا لَفِي الصُّحُفِ الْأُولَىٰ 
( 18 ) 
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
صُحُفِ إِبْرَاهِيمَ وَمُوسَىٰ 
( 19 ) 
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.