Swahili
Surah Abasa ( He frowned ) - Aya count 42
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ 
( 1 ) 
Alikunja kipaji na akageuka,
أَن جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ 
( 2 ) 
Kwa sababu alimjia kipofu!
وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُ يَزَّكَّىٰ 
( 3 ) 
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ الذِّكْرَىٰ 
( 4 ) 
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
أَمَّا مَنِ اسْتَغْنَىٰ 
( 5 ) 
Ama ajionaye hana haja,
فَأَنتَ لَهُ تَصَدَّىٰ 
( 6 ) 
Wewe ndio unamshughulikia?
وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ 
( 7 ) 
Na si juu yako kama hakutakasika.
وَأَمَّا مَن جَاءَكَ يَسْعَىٰ 
( 8 ) 
Ama anaye kujia kwa juhudi,
وَهُوَ يَخْشَىٰ 
( 9 ) 
Naye anaogopa,
فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ 
( 10 ) 
Ndio wewe unampuuza?
كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ 
( 11 ) 
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ 
( 12 ) 
Basi anaye penda akumbuke.
فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ 
( 13 ) 
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ 
( 14 ) 
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
بِأَيْدِي سَفَرَةٍ 
( 15 ) 
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
كِرَامٍ بَرَرَةٍ 
( 16 ) 
Watukufu, wema.
قُتِلَ الْإِنسَانُ مَا أَكْفَرَهُ 
( 17 ) 
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
مِنْ أَيِّ شَيْءٍ خَلَقَهُ 
( 18 ) 
Kwa kitu gani amemuumba?
مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُ فَقَدَّرَهُ 
( 19 ) 
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
ثُمَّ السَّبِيلَ يَسَّرَهُ 
( 20 ) 
Kisha akamsahilishia njia.
ثُمَّ أَمَاتَهُ فَأَقْبَرَهُ 
( 21 ) 
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
ثُمَّ إِذَا شَاءَ أَنشَرَهُ 
( 22 ) 
Kisha apendapo atamfufua.
كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَا أَمَرَهُ 
( 23 ) 
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
فَلْيَنظُرِ الْإِنسَانُ إِلَىٰ طَعَامِهِ 
( 24 ) 
Hebu mtu na atazame chakula chake.
أَنَّا صَبَبْنَا الْمَاءَ صَبًّا 
( 25 ) 
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
ثُمَّ شَقَقْنَا الْأَرْضَ شَقًّا 
( 26 ) 
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
فَأَنبَتْنَا فِيهَا حَبًّا 
( 27 ) 
Kisha tukaotesha humo nafaka,
وَعِنَبًا وَقَضْبًا 
( 28 ) 
Na zabibu, na mimea ya majani,
وَزَيْتُونًا وَنَخْلًا 
( 29 ) 
Na mizaituni, na mitende,
وَحَدَائِقَ غُلْبًا 
( 30 ) 
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
وَفَاكِهَةً وَأَبًّا 
( 31 ) 
Na matunda, na malisho ya wanyama;
مَّتَاعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ 
( 32 ) 
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَاءَتِ الصَّاخَّةُ 
( 33 ) 
Basi utakapo kuja ukelele,
يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ 
( 34 ) 
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
وَأُمِّهِ وَأَبِيهِ 
( 35 ) 
Na mamaye na babaye,
وَصَاحِبَتِهِ وَبَنِيهِ 
( 36 ) 
Na mkewe na wanawe -
لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ 
( 37 ) 
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ مُّسْفِرَةٌ 
( 38 ) 
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
ضَاحِكَةٌ مُّسْتَبْشِرَةٌ 
( 39 ) 
Zitacheka, zitachangamka;
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌ 
( 40 ) 
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ 
( 41 ) 
Giza totoro litazifunika,
أُولَٰئِكَ هُمُ الْكَفَرَةُ الْفَجَرَةُ 
( 42 ) 
Hao ndio makafiri watenda maovu.